• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
UVINZA DISTRICT COUNCIL
UVINZA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Idara/Vitengo
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mpango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo yaJamii na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi na Zima Moto
      • Maji
      • Usafi na Mazingira
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ugavi na Manunuzi
      • Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha Uongozi na Mipango
      • Mipango miji na mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Whe. Madiwani
      • Kuonana na Mhe. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayo Tekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti Mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo Mbalimbali
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Maji


IDARA YA MAJI

Idara ya maji ni moja kati ya Idara 12 za Halmashauri ya Uvinza na ilianzishwa rasmi tangu Julai, 2013 mara baada ya Halmashauri ya Uvinza kuanza. Idara ya Maji kwa sasa ina watumishi wa kuajiriwa wapatao 10.

MAJUKUMU YA IDARA

Idara ya Maji ikiwa ni moja ya Idara chini ya Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya inajishughulisha na kumsaidia/kumshauri Mkurugenzi Mtendaji Wilaya katika mambo yafuatayo:-

Kuandaa mipango na bajeti ya utoaji wa huduma ya maji kwa wananchi kwa mwaka.

Kuratibu shughuli za huduma ya maji Wilayani.

Kusimamia ujenzi wa miundombinu na ukarabati wake Wilayani.

Kutoa elimu na kuhamasisha wananchi juu ya usimamizi na uendeshaji wa miradi ya maji kwa maendeleo endelevu kwa kushirikiana na idara zingine.

Kuandaa taarifa na takwimu za huduma ya maji na kuziboresha kila wakati.

Mengineyo yanayojitokeza na kupangiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya.

MIKAKATI YA IDARA

Kuhakikisha huduma ya maji inaongezeka kutoka 44% iliyopo sasa mpaka kufikia 55 ifikapo Desemba, 2017.

Kuhakikisha miradi iliyopo inakuwa endelevu na inafanya kazi wakati wote.

Kuboresha taaluma ya watumishi ikiwa ni pamoja na maslahi yao.

Kuhakikisha Halmashauri inakuwa mstari wa mbele katika kuhudumia wananchi kwa ujumla

Takwimu za Maji Wilayani

Aina ya Teknolojia

Iliyojengwa 

Inayofanya kazi

Isiyofanya kazi

Visima vyenye mfumo wa jua

6

5

1

Visima vyenye pump za mikono

123

82

41

Miradi ya Maji Mtiririko

7

6

1

Miradi ya Maji ya Kusukumwa na Mashine

3

2

1

Jumla

139

95

44

Programu ya Maji Vijijini na Usafi wa Mazingira 

Serikali inatekeleza Programu ya Maji Vijijini na Usafi wa Mazingira. Programu hii inagharamiwa na Serikali pamoja na Wadau wa Maendeleo na inatekelezwa katika Wilaya zote nchini. Kwa Wilaya ya Uvinza vijiji 6 ndio vimeanza na vinaendelea na utekelezaji wa miradi ya Maji chini ya Programu hii ya Maji Vijijini na Usafi wa Mazingira.  Vijiji hivyo ni Uvinza, Nguruka, Ilagala, Kandaga, Rukoma na Kalya. Utekelezaji wa miradi hii umefikia hatua mbalimbali za ukamilishwaji.

Aidha miradi hii ikikamilika itawahudumia wananchi wapatao 110,770 na inategemewa kuongeza kiwango cha upatikanaji wa huduma ya maji hadi kufika asilimia 55. Mchanganuo wa miradi hiyo ni kama ulivyoonyeshwa hapa chini kwenye jedwali:-

Kijiji

Idadi ya Walengwa

Teknolojia 

Gharama ya ujenzi

Maelezo

Kandaga

12,107

Mradi wa kusukuma na mashine, magati 22

394,504,280

Ujenzi unaendelea
Rukoma

10,781

Mradi wa maji mserereko, magati 31

1,028,195,080

Ujenzi unaendelea
Nguruka

43,036

Mradi wa kusukuma na mashine, magati 55

2,873,196,856

Ujenzi unaendelea
Uvinza

9,346

Mradi wa maji mserereko, magati 26

1,713,969,015

Ujenzi unaendelea
Ilagala

25,799

Mradi wa kusukuma na mashine, magati 34

1,264,048,776

Uko hatua za mwisho
Kalya

9,701

Mradi wa maji mserereko, magati 28

777,777,343

Uko hatua za mwisho
Jumla

110,770

 

8,051,691,350        





Ofisi ya Jumuiya ya Watumia Maji Kalya ikiwa katika hatua za mwisho

Ujenzi wa tanki la 300m3 linalojengwa eneo la Nyangabo katika mradi wa Maji Nguruka

Shughuli ya umwagaji wa zege tanki la 500m3 katika mradi wa maji Nguruka ukiendelea

Shughuli ya umwagaji wa zege tanki la maji Nguruka ukiendelea

Ufungaji wa formwork katika tanki la 500m3 Nguruka

Tanki la 300m3 katika mradi wa maji Ilagala

Shughuli za ufungaji mabomba katika Mradi wa Maji kalya

Matangazo

  • HER YA SIKUKUU YA SABASABA July 07, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA SENSA July 18, 2022
  • TANGAZO WASIO NA NIDA July 19, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI July 25, 2022
  • Angaliza Zote

Taarifa za hivi Punde

  • Kilimo cha zao la PAMBA Uvinza

    March 22, 2023
  • Zoezi la ugawaji wa vitabu vya Mtaala Mpya -Uvinza

    March 16, 2023
  • Ukatili wa watoto ni urithi mbaya utatuangamiza na kututesa -RC Andengenye

    March 08, 2023
  • Serikali yakabidhi pikipiki 16 kwa Maafisa Ugani -Uvinza

    March 07, 2023
  • Angaliza Zote

Video

MAELEZO YA Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Uvinza na Mkurugenzi Mtengaji Kuelekea Nanenane 2020
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • News

Kurasa Mashuhuri

  • TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • Utumishi na Utawala Bora
  • TOVUTI YA MKOA WA KIGOMA
  • SALARY SLIP

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Uvinza - Lugufu Area

    Sanduku la Posta: P.O Box 12 UVINZA

    Simu ya Mezani: 0282988503

    Simu: 0757894484

    Barua Pepe: ded@uvinzadc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu
    • Sitemap
    • Huduma

Haki Miliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza . Haki zote zimehifadhiwa.