Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Eliamani Sedoyeka akiwa na Mkuu wa Wilaya Uvinza Mh. Dinnah Mathamani walipo hudhuria msiba nyumbani kwao marehemu Adam Harenga ambaye alikuwa Afisa misitu, katika Kijiji cha Bweru kata ya Itebula wilaya ya Uvinza, leo February 3,2023.
Akitoa salamu za pole, Prof. Eliamani amesema ‘kitendo cha kuwavamia, kuwapiga na kuwauwa ndugu hawa akikubaliki na nikitendo cha kikatili, na sisi kama serikali hatutakivumilia na tutahakikisha waliohusika wanakamatwa’
Marehemu Adam Harenga alivamiwa na kuuwawa January 31,2023 na kundi la wafugaji katika Hifadhi ya msitu uliopo Ilunde Kijiji cha Chakulu wakati akitekeleza majukumu yake ya kazi na wengine walio uwawa ni 2 kutoka jeshi la akiba.
Uvinza - Lugufu Area
Sanduku la Posta: P.O Box 12 UVINZA
Simu ya Mezani: 0282988503
Simu: 0757894484
Barua Pepe: ded@uvinzadc.go.tz
Haki Miliki©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza . Haki zote zimehifadhiwa.