Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kapt (Mst) George H. Mkuchika (Mb), leo tarehe 25, Septemba 2018 amefanya ziara ya kikazi katika wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma. Miongoni mwa shughuli alizofanya ni pamoja na kukutana na walengwa wa kaya masikini wanaohudumiwa na mfuko wa TASAF katika kata ya Kazuramimba Wilayani hapa.
Kabla ya kuelekea kata ya Kazuramimba alipata fursa ya kuongea na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza pamoja na watumishi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Uvinza katika Ukumbi wa Halmashauri.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Bw. Msongo Songoro alisoma taarifa ya Wilaya kwa Waziri huyo. Baada ya taarifa ya Kaimu Mkurugenzi, pia Mratibu wa TASAF ngazi ya Halmashauri alipata nafasi ya kusoma taarifa ya TASAF kwa Waziri. Hapo ndipo Mhe. Waziri alipoanza kuhoji matumizi na mgawanyo wa fedha za TASAF kwa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Uvinza. Fuatilia kilichotokea kupitia. >>> https://www.youtube.com/watch?v=vNiLVZ7np4M&feature=youtu.be
Uvinza - Lugufu Area
Sanduku la Posta: P.O Box 12 UVINZA
Simu ya Mezani: 0282988503
Simu: 0757894484
Barua Pepe: ded@uvinzadc.go.tz
Haki MilikiĀ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza . Haki zote zimehifadhiwa.